Posts

NISITIRI DhaminiHedhi Campaign – Kyela, Mbeya

August, 2020 Nisitiri Reusable Pads ziliwafikia mabinti wa wilaya ya Kyela mkoani Mbeya
Nisitiri Reusable Pads Kyela, Mbeya reach out.

Ilikuwa ni furaha kubwa sana kuweza kuwafikia mabinti hamsini (50) katika wilaya ya Kyela mkoani Mbeya na kuwapatia taulo za kike za Nisitiri.

Mmoja wa mabinti hawa aliileza timu nzima ya Nisitiri Project kwamba taulo hizi ni msaada mkubwa sana kwake kwani kabla ya hapo amekuwa akitumia magodoro yaliyochakaa pindi anapokuwa katika siku zake za hedhi ya mwezi.

Nisitiri Dhamini Hedhi campaign ni kwa ajili ya kuwasaidia mabinti ambao wanatoka katika familia maskini. Familia masikini ambazo hazina uwezo hata wa kukidhi mlo mmoja kwa siku hivyo kufanya suala la kumnunulia binti taulo za kike za kujisitiri wakati wa hedhi kuonekana kama ni anasa.

Campaign hii inahusisha kila mtu mwenye mapenzi mema na mabinti. Hedhi ni fahari ya mwanamke yeyote kwani humpa uhakika kwamba anacho moja kati ya vigezo muhimu sana cha kumpa sifa na uwezo wa kuongeza mwanadamu mwingine duniani.

Nisitiri Reusable Pads zinatayarishwa na LornaDadi Foundation na kutolewa bure kwa wanaufaika, yaani mabinti wenye uhitaji. Gharama za kutayarisha pakti moja ambayo ina taulo nne za kike (sanitary pads) ni kiasi cha TZS. 12,000/- tu. Hatuna mfadhili yoyote rasmi kwa ajili ya project hii bali ni watu mbalimbali (mtu mmoja mmoja) hujitolea kwa kununua hizi pakti kwa kadri wanavyowiwa.

Ikiwa unaguswa na campaign hii tafadhali wasiliana nasi kupitia simu nambari +255 786 666866 au tuma barua pepe kwenda lornadadi@gmail.com

Tunazidi kuwafikia mabinti mbalimbali kutoka sehemu tofauti tofauti za Tanzania. Na siku si nyingi tutaanza kukuletea simulizi za maisha yao ya ubinti hususani changamoto wanazozipitia wakati wa hedhi kupitia youtube channel yetu.

Asante kwa kutembelea website yetu.