Different talks

KUWA MWENYE FURAHA

Ni vizuri kuwa mwenye furaha! Je, unajua kuwa kuna njia nyingi unazoweza kujisaidia wewe mwenyewe kuwa mwenye furaha?

Hizi ni baadhi ya zile ambazo mimi huwa natumia kujisaidia kuwa mwenye furaha:

  1. Najitahidi kuimarisha uhusiano wangu na MUNGU nyakati zote: za vicheko ama vilio, raha ama huzuni, kukosa ama kupata, kupanda ama kushuka, nk.
  2. Kushughulisha akili yangu zaidi kwa mambo yanayoleta mtazamo chanya wa maisha
  3. Hupenda kuufanyisha mwili wako mazoezi, (nafanya mazoezi madogo madogo sana kwa wafanya mazoezi hawawezi kuyaita ya kwangu ni mazoezi).  Kufanya mazoezi huchangia sana kuwa na afya bora sio tu ya mwili bali na akili pia.
  4. Najitahidi kulala usingizi wenye utulivu. kwa watu wanaonijua wanasemaga “Lorna ana kifurushi cha kutosha cha usingizi”. Hii ni kwa sababu, linapokuja suala la kulala hata kama ni nusu saa tu mimi kwa kweli huwa nahakikisha nimelala. Na ninapolala akili yangu, moyo wangu, roho yangu na mwili wangu najitahidi sana viwe katika utulivu. Kuchoka sana kunaweza kuharibu hisia zako. Watu ambao hawana usingizi wa kutosha au hawapati usingizi tulivu wataalamu wanasema wapo kwenye hatari kubwa sana ya kupata tatizo la msongo wa mawazo.
  5. Najitahidi kupata mlo sahihi kwa wakati sahihi.  Mwili usipopata nguvu ya kutosha kwa kadri inavyohitajika kuna vitu havitaenda sawa katika mfumo mzima wa utendaji kazi wa mwili; hii huathiri hata uwezo au utendaji kazi wa akili ya mtu pia.
  6. Najitahidi kujenga mahusiano mazuri na watu tofauti kwa kadri ninavyokutana nao katika nyanja na hatua mbalimbali za maisha yangu. Naamini kwamba kuwa na mahusiano sahihi kunatengenezwa zaidi na kuwa na mawasiliano sahihi. Ninajitahidi kumweka kila mtu ninayekutana naye kwenye maisha yangu kwenye nafasi anayostahili kuwekwa na mimi ndani nyangu. Huwa nina akiba ya namna ninavyomchukulia mtu. Hii inanisaidia kujiepusha na vitu kama vile kumtarajia mtu awe wa aina fulani kwangu kumbe yeye kwangu mimi alivyojiweka ni tofauti na ninavyomchukulia.
  7. Ninalinda sana kile kilicho ndani yangu. Huwa siruhusu mtu yeyote aniburuze kwa namna yoyote ile; iwe hisia zangu, werevu wangu, nguvu zangu, maono yangu, moyo wangu au kitu kingine chochote kile ambacho kiuhalisia ni cha kwangu ambacho MUNGU ameweka ndani yangu. Huku Duniani kuna watu wanajua jinsi ya kurudisha watu wengine nyuma; anaweza kukufanya ukajihisi mjinga, huwezi kabisa kufanya chochote au ndoto uliyo nayo ni ujinga tu! Watu wa aina hii ukiwapa nafasi kwenye maisha yako ni rahisi sana kukubadilisha namna unavyofikiria kuhusu wewe mwenyewe. Unavyojifikiria kuhusu wewe mwenyewe ni nguzu muhimu sana ya maisha yako na kile kinachokwenda kudhihirika kwenye maisha yako. Ninaamini kwamba jinsi ninavyojisikia kujihusu na jinsi ninavyoamini kuhusu mimi mwenyewe huathiri sana mtazamo na imani yangu jinsi ninavyoamini kuhusu maisha na ninavyoyachukulia maisha kwa ujumla
  8. Ninatambua kwamba haijalishi nitafanya kitu chenye fedha nyingi kiasi gani au kunitanisha na watu maarufu kiasi gani au mimi mwenyewe kuwa maarufu kiasi gani, kama sitaishi maisha aliyonikusudia MUNGU kuishi hapa Duniani basi kamwe siwezi kuwa na furaha ya kweli maishani mwangu. Ninaamini kwamba, maisha yanayoweza kuni furaha ya kamili ni maisha ya kuziidhi ndoto zangu, maisha ya kuliishi kusudi la maisha yangu na maono MUNGU aliyoweka ndani yangu. Na nimechagua kukubali kwamba, jukumu la kutimiza maono yangu au ndoto zangu ni la kwangu mwenyewe.
  9. Siruhusu mtu yeyote yule au kitu chochote kile asimame au kisimame kama kikwazo cha mimi kutekeleza ninachopaswa kutekeleza ili kutimiza maono yangu. Na wala sihamishi jukumu la utekelezaji wa maono yangu au ndoto zangu kwa mtu mwingine yeyote yule.
  10. Ninaamini kwamba watu ambao MUNGU amewakusudia kuwa na mimi katika kutekeleza maono aliyoweka ndani yangu kwenye hatua tofauti tofauti za maono hayo, sio kila mtu ni sehemu ya ndoto au maono yangu haijalishi ni mtu wa karibu kwangu kiasi gani. Hii inanisaidi kuimarisha uhusiano wangu na watu wasionisapoti kwenye maono yangu.
  11. Naamini katika kusaidia weninge pale ninapoweza kufanya hivyo. Kusaidia watu wengine kunanipatia hisia za kusihi maisha yenye mguso kwa weninge hivyo kuniondolea kiburi cha kujiona mimi ni bora zaidi au ninastahili zaidi vitu fulani vya maisha kuliko kwengine. Ninaamini kwenye kutenda mema hapa Duniani.
  12. Najitahidi kuwa mwaminifu kwangu mwenyewe. Kwa kufanya hivi ninaweza kutimiza vitu vingi ambavyo nimejiwekea malengo mwenyewe. Nisipokuwa mwaminifu juu yangu au juu ya mambo yangu mwenyewe kamwe siwezi kuwa mwaminifu kwa watu wengine au mambo yanayohusu watu wengine.

Je ipo yoyote unayoona inakufaa katika ya hizo kumi na mbili?

Je, wewe unatumia njia gani au unafanya vitu gani kuhakikisha una furaha muda mwingi?

Niandikie hapo chini kwenye comment ili mimi na wengine tujifunze zaidi na kuboresha maisha yetu ya ndani.  Furaha ya kweli huboresha maisha yetu ya ndani.  Maisha yetu ya nje ni tafsiri ya maisha yetu ya ndani.

Andiko hili limepewa nguvu na kitabu cha Simulizi za “Vipande vya Maisha Vilivyopotea

MAFANIKIO YENYE USHAWISHI – II

ASILI YA MAFANIKIO

Katika mafanikio kuna vitu viwili ambavyo usipovielewa vinafanyaje kazi katika kuchangia wewe kupata mafanikio yako, utachanganyikiwa.  Vitu hivyo ni Sheria na Kanuni.

Fahamu:  Kuna sehemu ya Kanuni katika mafanikio au kutokufaniniwa kwa mtu binafsi na kuna sehemu ya sheria katika mafanikio au kutokufaniniwa kwa mtu binafsi.

Tofauti ya Sheria na Kanuni

Sheria zinaweza kukuzuia kufikia mafanikio unayotaka kuyafikia.  Yeyote anayetaka kufanikiwa ni lazima avunje sheria za maisha.  Kushindwa kwako katika maisha kunasababishwa na kitendo chako cha kuamua kuwa unatii sheria za maisha.  Usichanganye Sheria na Kanuni.

Kanuni za maisha

Kanuni za maisha hazifanyi kazi kulingana na kile ulichowahi kupitia katika maisha yako au unachopitia sasa, hapana.  Zinafanya kazi wakati wote, haijalishi kama unajua uwepo wa hizo kanuni au hujui.

Mafanikio yanatabirika na kushindwa pia kunatabirika kwa sababu kila kitu katika maisha kiliumbwa kufanya kazi kwa kanuni.  Kanuni huyafanya maisha kutabirika.  Kila kitu kina kanuni inayoambatana nacho kwa sababu kila alichoumba MUNGU kinapaswa kufanikiwa. Kila kitu kinafanikiwa kwa kufuata kanuni.  Kila mtu anafanikiwa kwa kufuata kanuni. 

MUNGU alimuumba mwanadamu kwa ustadi wa kiwango cha hali ya juu sana.  MUNGU aliweka kanuni ambazo endapo mwanadamu atazifuata ni lazima atafanikiwa.  Chochote alichokiumba MUNGU ni lazima kifanikiwe.  Mafanikio ni jambo zuri mbele za MUNGU.

Mafanikio ni muhimu.  Ukitaka kufanikiwa katika maisha usijaribu kufanikiwa katika maisha.  Watu wengi wanashindwa kufanikiwa kwa sababu wanajaribu kufanikiwa.  Watu waliofanikiwa hawakujaribu kufaninikiwa, walitekeleza kwa vitendo kanuni za mafanikio na kanuni za maisha.  Kwa maneno mengine, mafanikio ni matokea ya kuwa mtiifu kwenye kanuni.

Mafanikio ni matunda ya shughuli unayojihusisha nayo yaliyotokana na wewe kufuata kanuni.

Unajuaje kama umefanikiwa?

Mafanikio hayapimwi kwa kulinganisha jambo ulilofanya wewe na alilofanya mtu mwingine kwani siku zote wapo watu uliowazidi na waliokuzidi pia.  Mafanikio yanapimwa kwa kulinganisha kati ya kile ulichofanya na kile unachopaswa kufanya.  Mafanikio yanapimwa kupitia nia ya msingi ya wewe kufanya hicho unachofanya.  Mafanikio yako hayapimwi kutokana na kile ulichofanya, hapana, mafanikio yako hupimwa kutokana na lile kusudi la MUNGU kukuumba.  Mafanikio ni utimilifu wa kusudi la MUNGU juu ya maisha yako.  Mafanikio katika maisha yako yanachochewa na kusudi la MUNGU juu ya maisha yako, yaani kile kitu ambacho MUNGU alikuumba uje kukitimiza hapa duniani.  Mafanikio ni kutimia kwa mpango wa MUNGU juu ya maisha yako. Kuna kusudi MUNGU ameweka ndani yako na kuna mahali MUNGU anataka ufike. Haijalishi ni watu wangapi watakusifia, watakushangilia na kukupongeza, kama hukufanya kile kitu ambacho MUNGU anataka ufanye na kama hukufika pale ambapo MUNGU anapotaka ufike, wewe hujafanikiwa. Mafanikio ya Kiungu yanapimwa kwa kufikia ile hatima ambayo MUNGU amekukusudia.  Maisha sio kwa habari ya kufanya kazi kwa bidii lakini kufanya kazi kwa werevu na uhodari kwa kutumia maarifa sahihi.  Utaweza kufanya kazi kwa werevu ukiwa na maarifa yaliyofichwa kwenye kanuni. Chochote unachoanza kufanya au unachoacha kufanya kinategemea zaidi na kanuni unazozifuata au kutozifuata. Kufanikiwa kwako au kushindwa kwako kunategemea na kanuni za maisha unazotii au kutokutii.   Mafanikio sio suala la MUNGU bali ni juu yako wewe mwenyewe.

Mafanikio ni mchakato.  Mafanikio yanavutiwa zaidi na wewe kuwa unaenenda katika mwelekeo sahihi kuliko wewe kufika pale unapokwenda.  Mafanikio ni ule mchakato unaoupitia kuelekea kule unakotakiwa kufika na sio kufika kule unapotakiwa kufika.  Yaani mafanikio yanapatikana hapa njiani kwenye safari ya kuelekea kule unakotaka kufika.  Ukifanikiwa kwa kupitia mchakato sahihi unakuwa umetimiza kusudi lako.

Kama huzijui kanuni za hicho kitu unachotaka kufanikiwa ni dhahiri kwamba hutaweza kuzitii hizo kanuni, Unaposhindwa kuzitii hizo kanuni huwezi kufaninikiwa.  Haijalishi utajibidisha kwa kiwango gani au utamwomba MUNGU kwa kiasi gani.  Mafanikio ni matokea ya kutii kanuni.

Mafanikio yenye ushawishi ni yale yanayofuata kanuni.

—– Tutaendelea wiki ijayo.

Mafanikio Yenye Ushawishi

Ukifanikiwa katika kusudi la maisha yako unakuwa maarufu pia kwenye maisha ya watu mbalimbali.  Unapodhamiria kutimiza kusudi la maisha yako ni vyema utambue kwanza umuhimu wa kufanikiwa kwenye maeneo mengine yanayogusa maisha ya watu wengine. 

Hakuna kusudi la maisha la kutimiza pasipo kuona tatizo mahali fulani katika jamii inayokuzunguka. Hivyo ni wajibu wako kuangalia jamii inayokuzunguka na kuangalia ni changamoto ipi kati ya zilizoko katika jamii hiyo ambazo moyo wako unakusukuma kuitatua au kuwa sehemu ya utatuzi.  Mafanikio yanaanza kwa kuitambua changamoto fulani kwenye jamii na kuitatua.

Changamoto ni nyingi kwenye jamii zinazotuzunguka.  Kwa mfano, unaweza kukutana na mtu ambaye anatamani kufanya kile anachotakiwa kufanya lakini hafanyi.  Ni kitu gani unachoweza kumfanyia au kumsaidia mtu kama huyu? Kitu kimoja wapo ni kutumia karama na vipawa ambavyo MUNGU ameweka ndani yako kumsaidia huyu mtu kuziona fursa zinazomzunguka ambazo zinamuwezesha kufanikiwa kwenye kile anachotaka kufanya; lakini pia kumwezesha kuziona changamoto zilizokuwa zinamzuia yeye kufikia lengo lake.  Ukimsaidia kwa njia hii unakuwa umegusa maisha yake kwa namna fulani.

Sio kila wakati tunahitaji kuwa na pesa kuwasaidia watu kutoka kwenye changamoto zao. 

Muhimu:  Jitenge kutoka kwenye kundi la watu wanaoishi maisha ya kawaida, maisha yasiyokuwa na athari yoyote au mguso wowote kwenye jamii inayowazunguka.  Hama kutoka kwenye hayo maisha kwa kutumia kipawa na karama ulizo nazo.  Kuwa mtu mwenye ushawishi kwenye jamii.

Ushawishi ni uwezo wa kuwafanya watu wengine kukusikiliza au kufuatilia kile unachokifanya.  Unakuwa mtu mwenye Ushawishi pale ambapo watu wengine wanabadilisha vipaumbele vyao kwa ajili ya vipaumbele vyako.

Mafanikio yanakufanya uwe mtu mwenye ushawishi katika jamii.  Huwezi kufanikiwa mpaka uwe na ushawishi na huwezi kuwa na ushawishi mpaka umefanikiwa.  Vitu hivi vimeunganika na vinaambatana.

Ni nini asili ya mafanikio?

Tutaendelea wiki ijayo, usikose kutembelea ukurasa huu.

Imeandikwa na:

Lorna Dadi

Kwanini Huishi kwenye Kusudi la Maisha Yako?

Jaribu kufikiria jambo ambalo umekuwa ukitamani kulitimiza katika maisha yako lakini hujaweza kufanya hivyo.

Jambo ambalo lipo ndani kabisa ya moyo wako. Haijalishi ni kwa sababu gani hujaweza kulitimiza wewe litafakari tu.

Sio jambo la kushangaza, sisi wote nyakati flani katika maisha huwa tunateleza. Iko wazi tu hiyo. Wapo ambao wanaonekana kuwa bora kuliko sisi, hiyo ni kawaida tu kwani kuna ambao wanaonekana kutokuwa bora kama sisi.

Kwa kipindi ambacho nimekuwa nikijitolea kuzungumza na watu mbalimbali kuhusiana na changamoto wanazokutana nazo katika maisha, nimekuwa nikiulizwa ni changamoto gani kubwa ambayo nimeshakutana nayo katika maisha yangu. Huwa najitahidi kutokujibu hili swali kwani katika kila hatua ya maisha ninayopitia kuna changamoto zake.

Wengine wana matatizo ya mahusiano, wengine wana matatizo ya kifedha, wengine wana matatizo ya maradhi, nk Lakini tatizo kubwa nililokutana nalo kwa wengi wa hawa watu halikuwa na uhusiano wa moja kwa moja na masuala ya mahusiano, pesa, maradhi au vinginevyo. Tatizo lipo kwenye kile mtu anachokiamini ndani ya nafsi yake.

Ni rahisi kujua namna ya kumtongoza mtu, ni rahisi kujifunza namna ya kuanzisha biashara, ni rahisi kujifunza namna ya kufanya kitu ambacho unaogopa. Lakini sio rahisi kumudu hali yako ya kutokujiamini, nk ni ngumu sana kumudu HALI iliyopo ndani yako. Kumudu hali yako ya ndani kunahitaji uwekezaji thabiti.

Nguvu nyingi unazoweka kwenye eneo fulani la maisha yako zinaathiri (hasi au chanya) maeneo mengine ya maisha yako. Kwa mfano, kama una tatizo la kutokujiamini, ukiweka nguvu nyingi kwenye kupambana na hali ya kutokujiamini, utaweza kubadilishi maeneo mengine mwengi ya maisha yako (athari chanya) kwa kuwa utakuwa na moyo wa kuthubutu. Kanuni yoyote ya maisha huwa haina ubaguzi, hivyo hata kanuni ya kushindwa kutokana na kutokujiamini pia haina ubaguzi. Kutokujiamini kwako kutasababisha wewe kushindwa katika maeneo mengine ya maisha yako. Fikra za aina fulani unazojijengea akilini mwako zinakwenda kuwa shina kwenye maeneo mengine ya maisha yako. Kuwa makini na aina ya Fikra unazoruhusu kubebwa na akili yako.

Hata Fursa katika maisha huja kulingana na ile hali iliyopo ndani yako – aina ya Fikra zilizopo kwenye akili yako, au niseme kiwango cha utayari kilichomo ndani yako. Unapokumbana na fursa ambayo wewe unajikuta umechagua kuiita kuwa ni kubwa, wengi wetu huwa tunazikwepa. Fursa kubwa za maisha huja katika hali ambazo hatukuzitegemea. Fursa zikija na sura ngumu, mara nyingi tunachoweza kufanya ni kutafuta sababu lukuki za kukwepa yale maumivu ambayo ni lazima tuyapitie ili tutimize ndoto zetu kupitia hizo fursa.

Zifuatazo ni mbinu kumi za Kushindwa kufanya jambo ninavyofikiria mimi. Tutaanza na zile nyepesi na kumalizia na nzito zaidi. Karibu sana.

1. Huna ujasiri wa kusimamia kile unachokiamini katikati ya watu wanaokuzunguka

Popote pale duniani Jamii kama Jamii ina nguvu ya asili ambayo haikubaliani na Mwanajamii yeyote anayeonyesha kujitambua na kujiamini kuliko Wanajamii wenzake. Hii ni nguvu ya asili. Watu hawapendi wanapoona mtu mwingine anabadilika au anafanya kitu kinachowafanya wao wajisikie wako chini au yule mtu anang’aa zaidi yao. Kujituma kwa bidii ili kufikia ndoto zetu au ukuu wa kusudi la maisha yetu huwa inasababisha wale wanaotuzunguka kujisikia kutokuwa wakamilifu. Na kutokujisikia kwao kuwa wakamilifu kunakuja kwa njia tofauti ila njia kubwa ni wivu na kutukatisha tamaa. Unapojituma kufikia ndoto yako maana yake ni kuwasha taa kwenye ndoto zao zilizofunikwa ndani ya boga – kitu kikiwa ndani ya boga hakiwezi kuona mwanga wa nje. Kwa kifupi hawa watu wanaumia kwenye fikra zao. Inawafanya wajihoji sana kuhusu wewe, jambo ambalo sio watu wengi wanaweza kulimudu kwani mtu anatakiwa ajihoji kuhusu yeye mwenyewe na sio ajihoji kuhusu mtu mwingine.

Ukweli mdogo kuhusu maisha: Ukitaka kufanya kitu fulani cha tofauti lakini chenye mantiki ndani ya moyo wako, ni lazima uridhike na hali ya kuwa tofauti na watu wengine katika hiyo jamii. Kuna wakati watafikiri umechanganyikiwa, mbinafsi, una dharau, mzembe, mjinga, huna nidhamu, nk. Wale ambao umekuwa ukiwaona na kuamini kwamba wako karibu na wewe ndio hao hao watakao kuwa mwiba kwako. Kama hujajizungushia wigo imara kwenye unachokiamini na kuamua kukifanya au hauna uhakika na mawazo yako na matamanio yako, basi huwezi kufika mbali kwenye jambo hilo.

2. Huna Dhamira ya kutosha

Mwaka 2009 mwandishi Karl Marlantes alifanikiwa kutoa kitabu chake kiitwacho Matterhorn, kitabu kinachoelezea uzoefu kwenye vita za Vietnam. Kitabu kiliuzwa sana. New York Times walikinukuu kama kitabu pekee kikubwa na cha kushangaza kilichowahi kuandikwa kuhusiana na habari za kivita.

Ilimchukua Bw. Marlantes zaidi ya miaka 35 hadi kitabu chake kuchapishwa – yaani zaidi ya nusu ya umri wake. Aliandika mswada wa hicho kitabu mara sita. Kwa miongo miwili hakuna kampuni ya uchapishaji iliyokubali miswada hiyo na wengi wa makampuni hayo hawakutaka hata kusoma hiyo miswada.

Wengi wengi mara nyingi huwa tunakata tama mapema sana kwenye masuala ambayo tunatamani kufanikisha katika maisha yetu. Lakini, mtu yeyote ambaye amefanikiwa kupitia njia halali ana mlolongo wake wa jitihada na changamoto.

Ukweli mdogo kuhusu maisha: Mafanikio mazuri na mafanikio yenye historia. Historia yeyote ina nyakati ngumu na nyakati nyepesi. Ukitaka kufanikiwa ni lazima uwe tayari kukabiliana na nyakati zote.

3. Huna Unyenyekevu

Kuna watu waliotuzunguka wanaweza kufanya jambo dogo sana kwa ukamilifu na jamii inaamua kuwaita watu hawa “Wataalamu”. Unyenyekevu ninaomaanisha hapa ni kujua kile usichokijua

Katika ulimwengu wa biashara za mtandaoni, nimejifunza vitu vingi sana. Watu ambao wamekuwa waongeaji wazuri kuhusu mafanikio na wakati mwingine wakayakuza na hivyo kupata wafuasi wengi – wachache wana mafanikio ya wastani tu. Na wakati wengine hawajafanikiwa kabisa! Wengine bado ni tegemezi kwa watu wengine! Lakini bado wako radhi kujitapa kwa yeyote ambaye yupo tayari kuwasikiliza.

Lakini watu ambao wana utajiri halisi, utajiri uliotokana na kufanya kazi kwa bidii, utajiri uliopitia nyakati ngumu na nyepesi; ni mara chache sana kuwakuta wakiwa wanaongea ongea sana kuhusu kufanikiwa kwao, mara nyingi hupenda kuongelea kuhusu changamoto walinazokutana nazo katika mafanikio yao na jinsi gani walihitaji kujifunza zaidi kutokana na changamoto hizo.

Ukweli mdogo kuhusu maisha: Safari ya mafanikio inaambatana na changamoto nyingi, hizi changamoto unatakiwa uzione kama fursa ya kujifunza vile vitu ambavyo ulikuwa huvijui kwa sababu unataka kupata kitu ambacho ulikuwa huna ni lazima ujifunze vitu vipya vinavyoendana na hicho kitu ambacho unakitaka.

 

……… Tutaendelea namba 4-10 ………

Kuwa wa Tofauti

“Ili uwe tofauti na ulivyokuwa March 2017 ni lazima ufanye vitu vya tofauti au ufanye vitu vilevile lakini katika hali ya utofauti au ufanisi zaidi. Nazungumzia utofauti wenye mwelekeo chanya. Hili jambo tunaambiana kila siku ila wengi wetu wanashindwa kuchukua hatua sahihi.

Wakati Mungu anataka kukupeleka kwenye hatua nyingine mbele ili uweze kutimiza kusudi la maisha yako kuna vitu ni lazima uviache kama vile: Read more