NISITIRI DHAMINI HEDHI CAMPAIGN – Mchinga Experience

Tarehe 09.12.2020 kulikuwa na Kongamano la Wasichana kwenye ukumbi uliopo katika jengo la Jubilee Tower, jijini Dar es Salaam. Ni moja kati ya makongamano ya wanawake ambayo yalikuwa na mvuto mkubwa sana. Timu ya #NisitiriDhaminiHedhi kampeni ilishiriki kongamano hili pia.

09.12.2020 Nisitiri Dhamini Hedhi campaign awareness

Mh. Salma Kikwete alikuwa mgeni rasmi wa kongamano hilo. Baada ya kongamano kama ilivyo ada, alitembelea meza za wafanyabiashara mbalimbali waliokuwa nje ya ukumbi huo. Tulikuwa na meza kwa ajili ya #NisitiriReusablePads. Hatukuchukua meza kwa ajili ya biashara bali kwa ajili ya kuelemisha watu kuhusu changamoto wanayokutana nayo mabinti kutoka familia maskini wanapokuwa katika siku zao za hedhi.

Hon. Mama Salma Kikwete explaining something to LDF Member on 09.12.2020

Mama, Mh. Salma Kikwete aliziona taulo za kike za #Nisitiri na tukamwelimisha japo kwa ufupi ni namna gani zinaweza kumsaidia mtoto wa kike hasa kutoka familia yenye changamoto ya kiuchumi.  Alizifurahia na akatufahamisha kuhusu changamoto zilizopo katika jimbo la Mchinga.  Baada ya kutueleza akatukaribisha pia Mchinga ili tukajionee wenyewe na kuweza kuwasaidia mabinti wa eneo lile.

Tarehe 22.02.2021 tulipata neema na kibali kutoka kwa MUNGU kuweza kufika Manispaa ya Mchinga, wilayani Lindi katika mkoa wa Lindi. Tulipokelewa na ofisi ya Mkuu wa Wilaya, ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Mchinga, ofisi ya Mbunge wa Mchinga na mwakilishi wa WAMA Foundation (Taasisi isiyo ya Serikali inayoongozwa na Mh. Mama Salma Kikwete).

Tulitembelea shule mbili za sekondari; Kitomanga na Milola. Tulipata nafasi ya kuzungumza na walimu na wanafunzi.  Changamoto ni kubwa sana sio tu upatikanaji wa taulo za kile bali pia elimu sahihi kuhusu hedhi.

#NisitiriReusablePads distribution to Kitomanga Secondary School girls

Katika kila shule tulitoa zawadi ya boksi mia moja za #NisitiriReusablePads kwa ajili ya wanafunzi wa kike mia moja.

#NisitiriReusablePads distribution to Milola Secondary School girls

Girls at Kitomanga Secondary School with their gift of #NisitiriReusablePads

Watu wa Mchinga ni wakarimu sana.  Mchinga imetawaliwa na kijani kibichi.  Hali ya hewa ni nzuri sana.  Tulishuhudia maembe na nazi zilizoanguliwa zikiwa katika malundo malundo kwenye makazi ya watu mbalimbali wakati tukiwa tunaelekea Milola. 

Mchinga ni pazuri sana.  Tutarudi tena.